» » VIDEO: Sky Sports News wameripoti Man United kuwa na maamuzi haya kuhusu Jose Mourinho



Bado jina la kocha wa zamani wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho limekuwa likitajwa kwa ukaribu katika mbio za kuwania nafasi ya kocha wa sasa wa Man United Louis van Gaal, Mourinho amekuwa akiandikwa kwa zaidi ya miezi kadhaa sasa kama yeye ndio atakuwa mrithi wa Louis van Gaal msimu ujao.

Habari mpya zilizoripotiwa na Sky Sports News leo May 17 2016 ni kuwa kwa zaidi ya mwezi sasa uongozi wa klabu ya Man United umemthibitishia Jose Mourinho kuwa ndio atakuwa kocha wa Man United mwanzo mwa msimu, kama Louis van Gaal akiondoka ndani ya klabu hiyo.

Ripoti hiyo imeeleza kuwa Mourinho atakuwa na nafasi hiyo kutokana na Ryan Giggs ambaye ni kocha msaidizi kutopewa nafasi ya kufanya vizuri akiwa kama kocha wa timu hiyo, kwa muda mrefu sasa Louis van Gaal amekuwa akihusishwa kutaka kufukuzwa na Man United.

About Unknown

Hi there! I am Hung Duy and I am a true enthusiast in the areas of SEO and web design. In my personal life I spend time on photography, mountain climbing, snorkeling and dirt bike riding.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply